Psalms 81:1-3

Wimbo Wa Sikukuu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Asafu)


1 aMwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu;
mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!

2 bAnzeni wimbo, pigeni matari,
pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.


3 cPigeni baragumu za pembe za kondoo dume
wakati wa Mwandamo wa Mwezi,
na wakati wa mwezi mpevu,
katika siku ya Sikukuu yetu;
Copyright information for SwhKC